Jumatatu, 19 Desemba 2016

Hitaji La moyo



kama ajali ulikuja
Moyoni mwangu ukatua
Nikashindwa jizuia
Pendo langu nikakupa

Nikadhani nimepata
Mwandani wa kunifaa
Kumbe we ni shubiri
Uchungu wanipatia

Bila huruma waumiza
Ndani ya pendo hilo
Kwako mtumwa nikawa
Kwangu Ukawa mtwana

Mkali usiye huruma
Siku dakika pia saa
Bila kuchoka bila kusita
Kila huduma nilikupatia

Kwa sasa nimechoka
Njia yangu ninaenda
Asante kwa kunitesa
Moyo wangu kuuchoma

Mbali na mboni yako
Mbali na mateso yako
Sasa huru nimepata
Hitaji la moyo wangu
Moyo wangu utacheka

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni