*Kibamia meniponza*
Nilipika mboga yangu
Kisha nikatia nazi
Cheza na nyanya mafungu
Kuuonesha ujuzi
Kusudi isiwe chungu
Viungo vikawa Shazi
*Kibamia meniponza*
*Bora nisingekuweka*
Chumvi nikairamba
Ili radha kuionja
kisha nikajigamba
Bila sura kuikunja
Na kichwa kikanivimba
Nikajiona ni ninja
*Kibamia meniponza*
*Bora nisingekuweka*
Mboga ilipokaribia
Nikatoa mfuniko
Nikatia kibamia
Kiivie hukohuko
Yalokuja kutokea
Kweli ni mfadhaiko
*Kibamia meniponza*
*Bora nisingekuweka*
Kikaiharibu mboga
Sababu ya kuteleza
Nikaingiwa uoga
Jicho likawa kengeza
Nabaki kupiga soga
Ili muda kupoteza
*Kibamia meniponza*
*Bora nisingekuw eka*
Sifa mapishi ufundi
Chakula kiwe kitam
Uliza nani hapendi?
Chakula kitie ham
Usijetia mtindi
Kwenye nyama ni haram
*Kibamia meniponza*
*Bora nisingekuw eka*
✍🏿 Beatus kusaga
Reporter
Kasuku
0719368158